s

Chanzo cha picha, Getty Images

Liverpool wamevunja rekodi ya soka ya Uingereza baada ya kufikia makubaliano na Newcastle United kumsajili mshambuliaji wa Kiswidi, Alexander Isak, kwa ada ya £125m. Dili hili linamfanya kuwa mchezaji ghali zaidi katika historia ya Ligi Kuu England, likivunja rekodi ya usajili wa Florian Wirtz – £116m, iliyodumu muda mfupi, akisajiliwa msimu huu kutokea Bayer Leverkusen.

Isak anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya Jumatatu Septemba 01, 2025 kabla ya kusaini mkataba wa miaka sita Anfield. Liverpool walikuwa wamewasilisha awali ofa ya £110m mapema mwezi huu ambayo ilikataliwa, lakini mara hii wamerejea na dau kubwa zaidi lililowashawishi Newcastle kuachia mchezaji wao bora zaidi wa msimu uliopita.

Uhamisho huu unaashiria kutimia kwa malengo ya Liverpool chini ya kocha Arne Slot, ambaye alihitaji mshambuliaji mwenye kiwango cha juu ili kuendeleza mbio za kulinda taji la ligi. Kwa upande mwingine, Newcastle wanakabiliwa na changamoto za kifedha chini ya sheria za Financial Fair Play (FFP), hivyo dau hili kubwa limewapa nafasi ya kujipanga upya.

Kwa mashabiki wa Liverpool, usajili huu siyo tu taarifa njema , bali pia ni ishara kwamba klabu iko tayari kushindana na vilabu vinavyoongoza Ulaya. Kwa Arsenal ambayo imechapwa na Liverpool 1-0 katika mchezo wa ligi kuu Agosti 31, 2025 au Manchester CIty, hii ni changamoto mpya, kwani sasa wanakabiliana na timu ambayo imeongeza nguvu kubwa kwenye safu ya ushambuliaji.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *