.

Chanzo cha picha, Seenergy.ir

Maelezo ya picha, Mohammad Sadr ni mwanadiplomasia mkongwe ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wakati wa enzi ya mageuzi.

Baada ya vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran, baadhi ya wanasiasa na wataalamu nchini Iran waliibua wasiwasi kuhusu msimamo wa Urusi wakati wa vita hivyo, na ukosoaji huo umeendelea hadi leo.

Katika kadhia ya hivi punde zaidi, Mohammad Sadr, mjumbe wa Baraza la Utambuzi wa Mafanikio na Naibu Waziri wa zamani wa Mashauri ya Kigeni katika serikali ya Mageuzi hivi karibuni alidai kwamba “Huenda Urusi ikawa imeipatia Israel habari kuhusu mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran,” na katika muktadha huu, aliashiria usahihi wa mashambulizi ya Israel.

Katika matamshi yaliyochapishwa Septemba 1, 2025, kwenye chombo cha habari cha Synergy na video yake kupakiwa kwenye jukwaa la kushirikiana la Aparat, Bw. Sadr alisema: “Kuna mashaka kuhusu jinsi Israeli, katika vita vya hivi majuzi na katika migogoro ya hapo awali, ilivyokuwa na taarifa sahihi kuhusu vituo vyetu vya ulinzi wa anga. Kulingana na uchambuzi wangu, naweza kukuambia kwamba Warusi wameipatia Israeli habari muhimu.”

Alipoulizwa kama madai yake yalikuwa ya uchambuzi tu, Sadr alijibu: “Hii pia inatokana na habari.”



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *