.

Chanzo cha picha, Getty Images

Ndege aina ya Boeing B-29 ilikuwa mshambuliaji mahiri zaidi wa Vita vya Pili vya Dunia, na ilikuwa ghali zaidi kuiunda kuliko mabomu ya nyuklia iliyodondosha. Pia ilisaidia kushawishi ujenzi wa ndege za kubeba abiria zinazotumika hii leo.

Ilikuwa miaka miwili kabla ya shambulio la Japan kwenye Bandari ya Pearl kuiingiza Marekani kwenye vita. Lakini Jeshi la Anga la Marekani lilikuwa linatafuta ndege mpya kutumika katika mashambulizi.

Kilichofuata ni uundaji wa ndege aina ya “superbomber”, yenye uwezo wa kuruka hadi maili 2,000 (3,200km) kwa wakati mmoja na kwenye miinuko ambayo haikuwahi kufikiwa hapo awali.

Ndege waliyopata ilitupa mabomu ya atomiki huko Hiroshima na Nagasaki na hatimaye kukomesha Vita vya Pili vya Dunia.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *