Mwathiriwa aliyejeruhiwa katika tetemeko la ardhi akiwa amelala kitandani akiwa na bendeji kichwani na majeraha makubwa usoni akipokea matibabu katika hospitali ya Jalalabad, Afghanistan, tarehe 1 Septemba 2025.

Chanzo cha picha, EPA

Tetemeko baya la ardhi lililopiga mashariki mwa Afghanistan Jumapili jioni limeua mamia ya watu, kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Taliban. Wengine wengi wanadhaniwa kujeruhiwa.

Kitovu chake kilikuwa umbali wa kilomita 27 kutoka Jalalabad, mji wa tano kwa ukubwa nchini humo katika mkoa wa mashariki mwa Nangarhar mashariki mwa Afghanistan.

Likifikia ukubwa wa 6.0 kwa kina kirefu cha kilomita 8 – kiwango ambacho kinaweza kuusababisha haribifu zaidi kuliko ikiwachini zaidi – na kutikisa majengo kutoka Kabul hadi mji mkuu wa Pakistan, Islamabad.

Mnamo Juni 2022, tetemeko lingine la ardhi lenye ukubwa wa 6.1 lilipiga mashariki mwa Afghanistan na kuwaua zaidi ya watu elfu moja.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *