A head shot of Edgar Mwakabela taken from below with a scar around his jaw clearly visible.
Maelezo ya picha, Edgar Mwakabela alitekwa mwaka jana na kutelekezwa masituni baada ya kupigwa risasi ya kichwa

    • Author, Alfred Lasteck
    • Nafasi, BBC, Mbeya

Tahadhari: Makala hii ina maelezo ambayo baadhi wanaweza kuyaona ya kusikitisha!

Baada ya kutekwa akiwa amesimama kando ya moja ya barabara kuu katika jiji la Dar es Salaam, nchini Tanzania, mwanaharakati wa mitandaoni, Edgar Mwakabela, maarufu Sativa anasema aliponea chupuchupu kuuawa.

Anaeleza katika mahojiano na BBC namna gani baada ya kutekwa Juni 23, 2024 watekaji wake walimhoji na kisha kumsafirisha kwa zaidi ya kilometa 1,000 (maili 600), huku akipitishwa mikoa mbalimbali kabla ya kumtupa katika pori lililopo mkoani Katavi, jirani na mpaka wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).

Katika siku nne zilizofuata baada ya kutekwa, Sativa anasema alifungwa pingu, alifunikwa macho na kupigwa kikatili, ikiwemo kupigwa mara kwa mara kichwani, mgongoni na miguuni kwa kutumia ubapa wa panga.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *