Andre Onana

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Andre Onana

Manchester United wako tayari kumwachia kipa wa Cameroon Andre Onana, mwenye umri wa miaka 29, ajiunge na timu ya Saudi Arabia kwani dirisha la usajili kwa ligi hiyo bado liko wazi. (Teamtalk)

Kiungo wa Brazil, Casemiro (33), aliamua kubaki Old Trafford badala ya kwenda Al-Nassr ili kuongeza nafasi yake ya kucheza Kombe la Dunia 2026. (Goal)

Aliyekuwa kocha wa Tottenham, Ange Postecoglou, anatajwa kuwa miongoni mwa makocha wanaofikiriwa kuchukua nafasi ya Erik ten Hag huko Bayer Leverkusen baada ya Hag kutimuliwa kazi wiki hii (Sky Sports Germany)

Klabu ya Uturuki, Fenerbahce, iliyomtimua Jose Mourinho hivi karibuni, pia inaweza kuwa chaguo lingine la Postecoglou (60), ambaye aliipa Spurs ubingwa wa Europa League msimu uliopita kabla ya kutimuliwa. (Fabrizio Romano)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *