[ad_1]
Chanzo cha picha, Getty Images
Harry Maguire wa Manchester United na England, mwenye umri wa miaka 32, amekuwa akiwindwa na vilabu viwili vya Saudi Pro League na yupo tayari kufikiria uhamisho mwishoni mwa msimu huu. (Sun)
Mlinda mlango wa timu hiyo pia, Onana naye ameruhusiwa kwenda Uarabuni.
Mwenyekiti wa Crystal Palace Steve Parish alifanya mazungumzo ya ana kwa ana na beki wa England Marc Guehi, 25, pamoja na familia yake baada ya kusitisha uhamisho wa pauni milioni 35 kuelekea Liverpool. (Mirror)
Liverpool wanapanga kufanya majaribio ya kumnasa Guehi Januari na pia wanamtazama mshambuliaji wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ufaransa Michael Olise, 23, kama mrithi wa muda mrefu wa nyota wao wa Misri Mohamed Salah, 33. (Mail)
Bayern Munich nao wameingia kwenye kinyang’anyiro cha kumsajili Guehi, huku Real Madrid na Barcelona pia zikifuatilia kwa karibu suala lake. (Express)
Chanzo cha picha, Getty Images
Winga wa Liverpool na Uholanzi Cody Gakpo, 26, amesema Bayern Munich walikuwa wanamfuatilia kabla ya klabu hiyo ya Ujerumani kumsaini mshambuliaji wa Colombia Luis Diaz, 28, kutoka Liverpool badala yake. (ESPN)
Manchester United walijaribu kumsajili kiungo wa England Conor Gallagher, 25, kutoka Atletico Madrid katika siku za mwisho za dirisha la usajili wa majira ya kiangazi lakini wakakataliwa na klabu hiyo ya Hispania. (Fabrizio Romano, via FourFourTwo)
Tottenham walimfuatilia mshambuliaji wa Crystal Palace, Jean-Philippe Mateta, 28, raia wa Ufaransa, siku ya mwisho ya dirisha la usajili (Sky Sports)
Chanzo cha picha, Getty Images
Liverpool, Tottenham na Newcastle wote wanamfuatilia beki wa Brighton na Uholanzi Jan Paul van Hecke, 25, kwa usajili mwaka 2026. (Teamtalk), external
Juventus wanapima kama waendelee na mkataba wa Dusan Vlahovic, mshambuliaji wa Serbia mwenye umri wa miaka 25, ambao unamalizika msimu ujao. Kuanzia Januari ataweza kukubaliana na klabu nyingine. (La Gazzetta dello Sport)
Manchester United wapo tayari kusikiliza ofa kwa makipa wao; Altay Bayindir, 27, raia wa Uturuki, na Andre Onana, 29, raia wa Cameroon, kutoka vilabu vya Saudi Arabia na Uturuki. (Sun)
Monaco walikataa ombi la AC Milan kwa ajili ya beki wa Ujerumani Thilo Kehrer, 28, katika siku za mwisho za usajili. (Fabrizio Romano)
[ad_2]
Source link