Mwanamume aliyevaa shati ya hudhurungi amesimama mbele ya fani kupata unyunyu kutokana na joto kali

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Maelezo ya picha, Utafiti unaonyesha watu walio na viwango vya juu vya joto mara kwa mara wanazeeka haraka

    • Author, Angela Henshall
    • Nafasi, BBC World Service

Suleyman Hammudan amezoea kuishi katika jiji lenye joto kali mno.

Anajihusisha na mauzo ya teknolojia ya habari (IT) huko Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu, ambapo joto hupanda na kufikia zaidi ya nyuzi joto 45°C (113°F) kuanzia mwezi Juni hadi Septemba.

“Ukitembea nje wakati wa mchana, unahisi kana kwamba uko jangwani. Joto pamoja na unyevunyevu vinakuweka katika hali ya kukosa pumzi kabisa,” anasema.

“Kwa kawaida hufanya kazi nyumbani. Nikilazimika kutoka nje, huwa ni saa moja jioni jua linapotua lakini bado kuna joto, lakini si kali kiasi cha kushindwa kuvumilika.”



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *