.

Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images

Maelezo ya picha, Kamera za uchunguzi zilinasa wakati shambulizi la anga la Israel liliwalenga viongozi wa Hamas huko Doha, Qatar, Septemba 9, 2025.

Kundi la Hamas kutoka Palestina limetangaza vifo vya wanachama wake watano katika shambulio la anga la Israel kwenye mji mkuu wa Qatar, lakini likathibitisha kuwa jaribio la mauaji dhidi ya timu yake ya mazungumzo “limeshindwa.”

Hamas iliongeza kuwa timu ya mazungumzo ilikutana kujadili pendekezo la hivi punde la Marekani la kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza, wakati Israel ilipoanzisha mashambulizi ya anga ya kushtukiza yenye lengo la kuua ujumbe wa Hamas unaofanya mazungumzo huko Doha.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kwamba shambulio hilo kwenye makazi ya Qatar lilikuwa “halali” kwa sababu lililenga viongozi wakuu wa Hamas ambao, kulingana na Netanyahu, walipanga shambulio la Oktoba 7, 2023, dhidi ya Israeli, ambalo lilisababisha Vita vya Gaza.

Qatar ililaani shambulio hilo la Israel, na kulitaja kuwa la “uoga” na “ukiukwaji wa wazi wa sheria za kimataifa.”





Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *