Waandamanaji walikabiliana na polisi nje ya bunge huko Kathmandu, Nepal, Septemba 8, 2025, huku maelfu ya vijana wakiandamana kupinga marufuku ya serikali ya mitandao ya kijamii na ufisadi ulioenea.

Chanzo cha picha, Getty

    • Author, BBC News Nepali
    • Nafasi,
    • Author, Emily Atkinson
    • Nafasi, BBC News
    • Author, Iftikhar Khan
    • Nafasi, South Asia Regional Journalism

Waziri Mkuu wa Nepal, KP Sharma Oli, amejiuzulu kufuatia hasira kali ya umma baada ya vifo vya watu 22 waliouawa kwenye makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga ufisadi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi yake, kujiuzulu kwake kumelenga kufungua njia ya kupatikana kwa suluhisho la kikatiba kufuatia maandamano makubwa yanayoongozwa na vijana, yaliyosababishwa na tuhuma za ufisadi uliokithiri na marufuku ya mitandao ya kijamii ambayo sasa yameondolewa.

Maandamano hayo yaligeuka kuwa ya vurugu siku ya Jumatatu, baada ya maelfu ya waandamanaji wengi wao wakiwa wamebeba mabango yaliyokuwa na maandishi kuwa ni vijana wa kizazi cha Gen Z, Waliingia barabarani jijini Kathmandu.

Inakadiriwa kuwa watu takriban 200 walijeruhiwa katika makabiliano hayo, ambapo polisi walitumia gesi ya kutoa machozi, magari ya maji ya kuwatawanya waandamanaji, na hata risasi za moto.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *