Nuno Espirito Santo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Nuno Espirito Santo alikuwa meneja pekee mweusi aliyesimamia klabu ya Uingereza wakati wa kutimuliwa kwake na Nottingham Forest

    • Author, Sean Kearns
    • Nafasi, BBC Sport

Soka ya Uingereza iko hatarini kupoteza kizazi cha makocha wenye asili ya Kiafrika, Kiasia au mchanganyiko wa asili mbalimbali, kwa mujibu wa shirika la kupinga ubaguzi la Kick It Out.

Kutimuliwa kwa Nuno Espirito Santo na klabu ya Nottingham Forest wiki hii kunamaanisha kuwa kwa sasa hakuna tena meneja mwenya asili ya kiafrika anayesimamia klabu yoyote katika Ligi Kuu ya Uingereza.

Mara ya mwisho Ligi Kuu ya Uingereza kuwa bila meneja mwenye asili ya kiafrika ilikuwa kati ya mwezi Machi na Agosti 2023, baada ya kuondoka kwa Patrick Vieira kutoka Crystal Palace na kabla ya Vincent Kompany kupandisha Burnley daraja hadi ligi hiyo.

“Hili ni suala ambalo limekuwepo kwa zaidi ya muongo mmoja, na wapo wachezaji wa zamani waliokata tamaa ya kuwa makocha au mameneja,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Kick It Out, Samuel Okafor.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *