.

Chanzo cha picha, GP

    • Author, Na Laillah Mohammed
    • Nafasi, BBC Swahili
    • X,

Ni msimu wa siasa za uchaguzi katika mataifa ya Afrika Mashariki. Tanzania ikiwa inatarajiwa kuandaa uchaguzi mkuu Oktoba 29 mwaka huu nayo Uganda ikiifuata nyuma mnamo Januari 12 2026. Kenya bado ina muda, kwani inatarajiwa kuandaa uchaguzi mkuu Agosti 2027.

Na japo Kenya ina miaka miwili kabla ya kuandaa uchaguzi mkuu, vijana kadhaa wamejitokeza na kutangaza rasmi azimio lao la kumrithi Rais William Ruto.

Pia unaweza kusoma

Uchaguzi Mkuu Kenya 2027

Idadi ya watia nia wenye matarajio ya kumuondoa madarakani Rais William Ruto inaongezeka kila uchao nchini Kenya, jambo ambalo baadhi ya wachambuzi wa siasa wanahisi huenda likaleta changamoto kubwa kwa juhudi za kumng’atua madarakani kupitia kura.

Ruto ambaye atakuwa anawania kiti hicho kwa awamu ya pili atamenyana na vijana wenye umri ulio chini ya miaka 45 ikiwa vijana hao watatimiza kanuni za tume huru ya uchaguzi nchini Kenya IEBC.





Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *