Hatua ya kuwarejesha nyumbani wawakilishi hao wa kidiplomasia Iran imechukuliwa saa kadhaa baada ya juhudi za Urusi na China za kuchelewesha kufufua vikwazo dhidi ya Iran kugonga mwamba Ijumaa mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Hofu ya Umoja wa Mataifa kuiwekea tena vikwazo Iran

Hayo yanajiri wakati Umoja wa Mataifa ukitazamiwa kuiwekea vikwazo vikali Iran Jumamosi  27.09.2025 baada ya mazungumzo ya nyuklia kati ya taifa hilo na mataifa ya magharibi kukwama. Vikwazo hivyo vitakapotangazwa vinatazamiwa kuanza kufanya kazi kuanzia Jumapili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *