Haya ni mashambulizi ya hivi karibuni kutokea ya vita kati ya  jeshi la taifa na wanamgambo wanaotaka kuudhibiti mji huo.

Kamishna Mkuu wa Haki za Binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk, amesema eneo jirani na mji huo la Daraja Oula umekuwa ukishambuliwa mara kwa mara na RSF kupitia mashambulizi ya droni na ya ardhini kati ya Septemba 19 na 29.

Türk ametaka hatua za haraka kuchukuliwa ili kuzuwia mateso na mashambulizi ya kikabila mjini El Fasher. Wanamgambo hao hadi sasa bado hawajatoa maoni yoyote kuhusiana na taarifa hiyo.

Kulingana na takwimu shirika la afya ulimwenguni WHO, mapigano ya wenyewe kwa wenyewe Sudan kati ya RSF na jeshi la taifa yalioanza mwaka 2023 yamesababisha mauaji ya watu 40,000 huku wengi zaidi ya milioni 2 wakiachwa bila makao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *