WHO imesema watu wengine 64 walithibitishwa kuambukizwa ugonjwa huo, lakini ikasema kuwa hatari ya Ebola kuenea katika eneo hilo ni ndogo.

Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema shirika lake pamoja na washirika wake wanaendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya DRC za kuudhibiti ugonjwa huo.

Wiki mbili zilizopita wizara ya afya nchini Kongo ilianza kutoa chanjo dhidi ya Ebola.

Ugonjwa huo unaoambukizwa kupitia majimaji ya mwili umewauwa watu 15,000 barani Afrika ndani ya miongo mitano iliyopita.

Mripuko wa ugonjwa huo nchini Kongo kati ya mwaka 2018 na 2020 ulisababisha vifo vya takriban watu 2,300

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *