
Kulingana na mamlaka nchini humo, Urusi ilifanya mashambulizi kwa kutumia droni 381 na makombora 35 yaliyoilenga miundombinu hiyo kwenye mikoa ya Kharkiv na Poltava iliko mitambo mikubwa ya kuzalisha gesi.
Shughuli za kampuni ya mafuta na gesi za DTEK zasitishwa
Kufuatia mashambulizi hayo, Kampuni kubwa zaidi binafsi ya mafuta na gesi ya Ukraine DTEK imetangaza kupitia jukwaa la X kuwa sitisha shughuli zake katika baadhi ya vituo vyake katika mkoa wa Poltava baada ya mashambulizi ya Urusi.