Takriban waandamanaji 1,000 waliandamana dhidi ya serikali katika mji mkuu wa Antananarivo nchini Madagascar, Alhamisi, wakimtaka Rais Andry Rajoelina ajiuzulu.

Maandamano hayo yalifanyika wakati wa machafuko makubwa zaidi kuwahi kufanyika nchini Madagascar, ambapo polisi walitumia mabomu ya machozi, na risasi za mpira kutawanya umati wa waandamanaji.

Maandamano hayo, yanayoendeshwa na kizazi cha “Gen Z Madagascar,” muungano wa wanafunzi na vijana, yalichochewa na hasira kutokana na kukatika kwa huduma za maji na umeme, lakini baadaye yaligeuka kuwa maandamano ya kumtaka Rais Rajoelina ajiuzulu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *