Jeshi la Guinea-Bissau limetangaza kuwa lilitibua jaribio la mapinduzi siku ya Ijumaa lilohusisha maafisa kadhaa, kulingana na vyombo vya habari.

Majenerali wa jeshi wamejitokeza katika mkutano na waandishi wa habari mubashara na kushtumu “jaribio linginge na kukiuka utaratibu wa katiba” kabla ya uchaguzi ulioratibiwa kufanyika Novemba 23.

Naibu Mkuu wa Majeshi Jenerali Mamadu Ture amesema uchunguzi unaendelea na wote waliohusika watakamatwa, Shirika la habari la Guinea-Bissau, Capital News limeripoti.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *