Changamoto zinazoendelea

Baada ya tishio la Trump, Rais Tinubu alisema serikali yake iko tayari kushirikiana na washirika wa kimataifa kutatua changamoto za usalama.

Hata hivyo, wataalamu wanasema hali ni ngumu — vurugu zimekuwa zikijirudia kwa miongo miwili, na jeshi limezidiwa kutokana na mapambano katika maeneo mengi.

Jeshi la Nigeria linapambana na Boko Haram kaskazini mashariki, makundi yanayohusiana na Al Qaeda kaskazini magharibi, na magenge ya majambazi katikati mwa nchi.

Idadi ya wanajeshi haijaongezeka kulingana na ukubwa wa changamoto, huku polisi wakiwa wachache na wasio na vifaa vya kutosha.

“Jeshi la Nigeria bado halina vifaa vya kisasa, silaha, wala uwezo wa kijasusi wa kutosha,” asema Bukarti.

“Pia kuna upungufu mkubwa wa ushirikiano kati ya taasisi nyingi za usalama, zaidi ya taasisi 17, ambazo zote zina jukumu katika kurejesha amani.”

Hofu ya kukabiliana na Trump

Kutajwa kama nchi yenye inayowapa Marekani wasiwasi ni pigo kubwa kwa Nigeria, na linaweza kuwa na athari mbaya zaidi kwa uchumi wake ambao tayari uko katika hali mbaya.

Wataalamu wanasema kurekebisha uhusiano na serikali ya Trump kutahitaji Abuja kuchukua hatua za kidiplomasia kwa utulivu.

“Serikali ya Nigeria inapaswa kuwa na busara, isiingie kwenye malumbano ya maneno. Ni bora ijihusishe kidiplomasia na Marekani, ionyeshe kwamba Waislamu na Wakristo wote ni waathirika wa vurugu, na iombe ushirikiano katika silaha, mafunzo na ujasusi,” asema Bukarti.

Msemaji wa Rais wa Nigeria ameeleza kuwa madai ya Trump yalikuwa “mawasiliano yaliyopotoshwa”, akitumaini kuwa viongozi wa mataifa hayo mawili wataweza “kutatua tofauti zao”. 

Mtazamo wa kibiashara wa Trump

Utawala wa Trump umekuwa ukifanya makubaliano na baadhi ya nchi za Afrika kukubali wahamiaji waliorejeshwa kutoka nchi zingine katika juhudi za kudhibiti uhamiaji haramu.

Ghana, Eswatini, Rwanda na Sudan Kusini zimepokea wahamiaji hao, huku Uganda ikikubali makubaliano lakini bado haijampokea yeyote.

Nigeria ilikataa kushiriki katika mpango huo, jambo ambalo wachambuzi wanalihusisha na kupotea kwa uhusiano mzuri kati yake na utawala wa Trump.

Wataalamu wanasema mtindo huu wa “diplomasia ya kibiashara” unalenga kuwashinikiza viongozi wa Afrika, mbinu ambayo Trump pia aliitumia dhidi ya Afrika Kusini kwa madai ya “mauaji ya wazungu”, madai ambayo serikali ya Pretoria imeyakanusha kama ya uongo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *