
Ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Afrika ulisema hapo jana waangalizi wake walishuhudia wapiga kura wakipewa kura nyingi, huku baadhi wakiruhusiwa kupiga kura zao bila utambulisho wao kuthibitishwa katika orodha ya wapiga kura kwenye daftari la wapiga kura huko Tanzania.
Ripoti ya awali kutoka kwa ujumbe wa Umoja wa Afrika inasema uchaguzi mkuu wa Tanzania wa 2025 haukuzingatia kanuni za Umoja wa Afrika, mifumo ya kanuni, na majukumu na viwango vingine vya kimataifa vya uchaguzi wa kidemokrasia.
Ujumbe huo ulisema waangalizi wake walizuiliwa kufuatilia hesabu ya kura, ikibainisha kuwa uwazi ulibanwa. Ripoti iliongeza kusema katika baadhi ya vituo vya kupigia kura waangalizi waliombwa kuangalia upigaji kura kwa dakika tano pekee.
Ripoti hiyo pia ilibainisha maandamano ya vurugu, milio ya risasi, kufungwa kwa barabara, na kuchomwa kwa matairi katika maeneo kama vile Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kagera, Dodoma, Kigoma, Tebora, Buhungwa, Singinda, miongoni mwa mengine.
Umoja wa Afrika umeitaka Tanzania kuyapa kipaumbele mageuzi ya sheria za uchaguzi na kisiasa ili kushughulikia sababu kuu za changamoto zake za kidemokrasia na uchaguzi.