
Kujiuzulu kwa Jaji Yusuf, kuanzia Septemba 30, 2025, kulitoa nafasia kwa jopo hilo la majaji 15 wa ICJ, ambayo iko The Hague, Uholanzi.
Okowa alipata kura 106 kati ya 185 katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, na kupita kiwango cha kura 97 na alipata kura nane kati ya 15 za Baraza la Usalama, idadi ya chini inayohitajika ili kuchukua nafasi hiyo.
Aliteuliwa kwa pamoja na Colombia, Kenya, Namibia, Uholanzi, Romania, Afrika Kusini, Sweden, na Vanuatu. Atakuwepo kwenye nafasi hiyo hadi Februari 5, 2027, muda uliosalia wa kipindi cha Jaji Yusuf.
Okowa anakuwa Mkenya wa kwanza kuhudumu kama jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki, na hivyo kuashiria hatua ya kihistoria kwa taifa hilo na kanda.
Sasa anajiunga na jopo lililochaguliwa la wanasheria wa Kiafrika ambao wamehudumu katika Mahakama, akiwemo Abdul Koroma wa Sierra Leone na Abdulqawi wa Somalia.
Uchaguzi wake unaimarisha zaidi uwakilishi wa Kenya katika vyombo vya juu vya sheria vya kimataifa, ikiwa ni pamoja na Tume ya Kimataifa ya Sheria, ambako amehudumu pia.