
Baraza hilo la Maaskofu limeorodhesha matakwa yao katika taarifa hiyo ikiwemo kuwataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wote waliohusika na mauaji wawajibike au kuwajibishwa na mamlaka zao za uteuzi.
Katika orodha ya vitu vinane walivyotaka vifanyike, pia wameitisha wale wote waliokamatwa kwa hila kabla na baada ya uchaguzi na kuwekwa mahabusu au mahali pasipojulikana waachiwe huru na bila ya masharti yoyote.
Tume ya kuchunguza mauaji
‘‘Katiba mpya na utawala wa sheria vimekuwa kilio cha muda mrefu hapa nchini. Mchakato wa Katiba mpya yenye kujali utu, usawa, haki, ukweli kwa wote uanze kwa kukushirikisha wadau wote. Ili tusirudi tena katika machafuko na nchi iongozwe katika utawala wa sheria.’’ wameongeza.
Tanzania imetumbukia katika lawama na shutuma za kimataifa tangu Oktoba 29, ambapo maandamano ya kupinga uchaguzi mkuu yalikabiliwa kwa nguvu kupita kiasi, huku vijana wengi wakidaiwa kuuawa kw akupigwa risasi na vyombo vya uslama.
Awali uongozi wa serikali ulikanusha madai kuwa Watanzania waliuawa, lakini baadaye, katika hotuba ya kwanz aya kulifungua bunge Rais Samia Suluhu Hassan, alitangaza kuteua tume itakayofanya uchunguzi huku akitoa pole kwa waliofiwa na waliojeruhiwa katika maandamano.