
Katika taarifa, Arsenal ilikiri mchango mkubwa wa ushirikiano huo. Msemaji wa klabu alisema, “Uhusiano wetu na Visit Rwanda umekuwa sehemu muhimu ya mkakati wetu wa kibiashara kimataifa. Tumefanikiwa kufanya mambo makubwa pamoja, kuanzia programu za kijamii hadi kuongezea mwonekano wa Rwanda duniani.”
Kwa upande wa Rwanda, mafanikio ya ushirikiano huo yalisisitizwa pia. Mwakilishi wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda alisema, “Tulipoanza safari hii, lengo letu lilikuwa kuutambulisha utalii wa Rwanda kwa dunia. Kilichopatikana katika ushirikiano huu, ongezeko la watalii, kutambulika kimataifa, na ushirikiano wa kitamaduni — kilizidi matarajio yetu. Tunashukuru Arsenal kwa miaka nane yenye mafanikio.”