Mauaji ya halaiki Gaza

Akizungumzia mauaji ya halaiki yanayoendelea Gaza, Erdogan alisema: “Kama familia ya wanadamu, deni letu kubwa kwa watu wa Palestina ni haki. Njia ya kulilipa deni hili ni kutekeleza suluhisho la mataifa mawili kulingana na mipaka ya mwaka 1967.”

“Naamini tutaendelea kuchukua hatua za pamoja dhidi ya vitendo vyovyote vya uhasama vinavyoweza kuathiri utambulisho wa kihistoria wa Jerusalem Mashariki,” aliongeza.

Erdogan alisema jeshi la Israel linashambulia maeneo ya raia huko Gaza, ikiwa ni pamoja na makanisa na misikiti, akibainisha kuwa miongoni mwa maeneo ya ibada yaliyoathiriwa ni Kanisa la Holy Family la Gaza, linaloendeshwa na Kanisa Katoliki.

Alisisitiza kuwa “kulinda hali ya kihistoria iliyozoeleka” katika Mji Mtakatifu wa Jerusalem ni jambo la “umuhimu mkubwa sana.”

“Chanzo cha utulivu”

Kwa upande wake Papa alisema Uturuki ina nafasi muhimu katika hali ya sasa na ya baadaye ya eneo la Mediterania na dunia nzima, akiipongeza nchi hiyo kwa kuthamini utofauti wake wa ndani.

Akitoa wito kwa Ankara kukubali jukumu lake kama mpatanishi katika ulimwengu uliokumbwa na mizozo, alisema: “Mheshimiwa Rais, naomba Uturuki iwe chanzo cha utulivu na maelewano kati ya watu, katika huduma ya amani ya haki na ya kudumu.”

“Leo kuliko wakati mwingine wowote, tunahitaji watu ambao watakuza mazungumzo na kuyafanyia kazi, kwa nia thabiti na suluhu la subira,” alisema Leo, akiashiria kuongezeka kwa nafasi ya Uturuki katika juhudi za utatuzi wa migogoro huko Gaza, Ukraine na kwingineko.

Papa Leo pia alionya kwamba migogoro ya kimataifa inaweza kufungua njia kwa ajili ya vita ya tatu ya dunia, akisema, “mustakbali wa wanadamu uko hatarini,” na “hatupaswi kushindwa kwa njia hii.”

Aliongeza kuwa baada ya maafa ya vita viwili vya dunia, ambavyo vilishuhudia kujengwa kwa mashirika makubwa ya kimataifa, “sasa tunapitia awamu inayoashiria kiwango cha juu cha migogoro katika ngazi ya kimataifa, inayochochewa na mikakati iliyopo ya nguvu za kiuchumi na kijeshi.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *