Rais wa Israel Isaac Herzog, amesema kuwa ombi la Waziri Mkuu wan chi hiyo Benjamin Netanyahu, kupata msamaha kwenye kesi yake ya ufisadi litazua mjadala.

Akizungumza siku ya jumatatu, Herzog alisema ombi hilo litashughulikiwa kwa uangalifu mkubwa.

“Nitazingatia maslahi ya Israel na jamii ya Waisrael,”alisema Herzog kupitia taarifa ya ofisi yake.

Kulingana na Herzog, uamuzi huo utaibua sintofahamu na hoja tofauti nchini humo.

“Ila kitu kimoja kilicho dhahiri kwangu, huwa sishawishiki na uovu wowote,” alisema Herzog.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *