Watu wapatao 37 hawajulikani walipo baada ya boti kuzama mtoni kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Tukio hilo lilitokea Mto Luangatshimo Jumatano iliyopita, na kuja kuthibitishwa na vyombo vya habari Jumatatu.
Chombo hicho kilikuwa na abiria 42 wakati kikitokea mji wa Lovua kuelekea Nangalula, kabla hakijapoteza muelekeo katika yam to huo, kulingana na afisa wa eneo hilo, aliyejitambulisha kama Nico Ngenza Kitambala.