Klabu ya soka ya Tanzania, Simba imesitisha mkataba na aliyekuwa meneja mkuu Dimitar Pantev pamoja na wasaidizi wake wawili.

Kulingana kwa taarifa ya umma iliyotolewa na Simba Sports Club kupitia ukurasa wake wa X (zamani twitter), Simba imefikia makubaliano hayo ya pande mbili, huku kikosi hicho sasa kikiwa chini ya kocha Selemani Matola, wakati mchakato wa kutafuta kocha mwingine ukiendelea.

Uamuzi  huo unakuja siku mbili baada ya Simba Sports Club kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Stade Malien ya Mali, katika mchezo Kundi D wa Ligi ya Mabingwa Afrika, uliofanyika Novemba 30 mjini Bamako.

Kabla ya hapo, timu hiyo ilipoteza nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Petro de Luanda ya nchini Angola.

Pantev alichukua mikoba ya kuwafundisha ‘Wekundu wa Msimbazi’ mwezi Oktoba 2025, akitokea Gaborone United ya Botswana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *