Uturuki imesisitiza haja ya jamii ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya hatua za Israel katika eneo hilo.

Israel imeendeleza uvamizi wake katika Ukingo wa Magharibi na Jerusalem inayokaliwa na kuendeleza sera za kujitanua zenye lengo la kuyumbisha Syria na Lebanon, msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa Zeki Akturk alisema katika mkutano na waandishi wa habari wa kila wiki siku ya Alhamisi.

“Kwa mara nyingine tena tunasema kwamba jamii ya kimataifa, kwanza kabisa Umoja wa Mataifa, lazima ionyeshe nia iliyoimarika na inayoweza kutekelezeka na kuchukua hatua dhidi ya hatua za Israel zinazotishia amani na utulivu wa kikanda,” alisema.

Amesisitiza haja ya kufikishwa salama kwa misaada ya binadamau bila ya kuzuiliwa huko Gaza, usambazaji wa mahitaji ya dharura ya kiraia na utekelezaji kamili wa masharti ya usitishaji vita.

Kuhakikisha haya, alisema, ni muhimu kwa utulivu wa kikanda, na kuongeza kuwa Uturuki itaendelea kuunga mkono juhudi zote za kujenga za kimataifa.

Akturk pia aliangazia nafasi ya Uturuki katika NATO, akibainisha kuwa nchi hiyo imetimiza majukumu yake yote kwa mafanikio tangu kujiunga na Jumuiya hiyo mnamo 1952.

“Kama matokeo ya diplomasia ya Uturuki na jukumu kubwa la kimataifa linaloungwa mkono na shughuli za kijeshi za pande nyingi, Mkutano wa Viongozi wa NATO utafanyika Ankara mnamo Julai 2026,” alisema.

Programu ya mkutano huo pia itajumuisha Jukwaa la Sekta ya Ulinzi na Mkutano wa Mawaziri wa Ulinzi wa NATO.

Aliongeza kuwa matukio mawili ya ziada ya ngazi ya juu ya NATO yataandaliwa Uturuki mwaka huo huo.

Mkutano wa Wadau wa NATO, unaozingatia mbinu za mawasiliano ndani ya mazingira ya sasa ya usalama na ubunifu katika mawasiliano ya kimkakati, utafanyika Istanbul mnamo Septemba.

Wakati huo huo, toleo la tatu la NATO EDGE, lililoandaliwa chini ya Shirika la Mawasiliano na Habari la NATO (NCIA) na kuangazia mada kadhaa ikiwemo akili mnemba na usalama wa mtandao hadi mifumo ya udhibiti na teknolojia ya kushiriki data, itafanyika Izmir mnamo Novemba 17-19 2026.

Akturk alisema Kikosi cha Wanajeshi wa Uturuki (TAF) kiliendelea na shughuli zao za mafunzo na mazoezi kwa mafanikio, akibainisha ushiriki wa Uturuki katika zoezi la Loyal Dolos la NATO nchini Poland.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *