Mwezi Juni 2025, mapatano ya awali ya amani yalitiwa saini na mawaziri wa Mambo ya Nje wa DRC na Rwanda mjini Washington.

Kumuondoa China katika biashara wa madini

Chini ya mkataba mpya na Marekani, DRC sasa inatakiwa kutoa orodha ya awali ya rasilimali muhimu za madini, na maeneo ambayo hayana leseni kama sehemu ya Hifadhi yake Mali ya Kimkakati. Itatakiwa kutoa orodha hii ndani ya siku thelathini (30) baada ya kuanza kutumika kwa Makubaliano haya.

Wakati wowote, rasilimali muhimu za ziada za madini, rasilimali za dhahabu, na maeneo yasiyo na leseni yanaweza kuongezwa na DRC kwenye orodha hii. Na udhibiti wa maelezo haya yatakuwa chini ya kamati ya pamoja itakayoundwa kati ya Marekani na DRC.

“Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inajitolea kutekeleza, kwa dhati kabisa, majukumu yote yanayotokana na Makubaliano haya,” Felix tshisekedi, Rais wa DRC alisema.

“Tutafanya hivyo kwa umakini, kwa ukali, na kwa kujali mara kwa mara amani, usalama wa watu wetu.”

Lakini wataalamu wanasema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Marekani wa kupunguza utegemezi kwa China, ambayo kwa sasa inadhibiti zaidi ya 70% ya uchimbaji madini adimu duniani na zaidi ya 85% ya usindikaji.

Nchini DRC, China imekuwa ikifua madini, hasa kobalti tangu mwaka 2008, ilipofanya makubaliano na serikali ya DRC yaliyoitwa mkataba wa Sino Congolaise des Mines (Sicomines).

Walakini, mikataba hii ni ya masharti.

Ushirikiano wa kiuchumi utaanzishwa kikamilifu ikiwa tu usitishaji wa mapigano utaendelea na uondoaji wa kijeshi utaheshimiwa.

Na huku Marekani ikijitayarisha kupelekea makampuni yake makubwa kufua madini nchini DRC, maelfu ya watu wanaoteseka kutokana na kutokuwepo na usalaama nchini DRC, wamebaki bila kuelewa makubaliano haya mapya ya Washington yatarudisha vipi hali ya usalama na utulivu maishani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *