Katika mazungumzo hayo, Putin analenga kuongeza biashara na India ambayo ndiyo mnunuaji wake mkubwa wa silaha na mafuta, wakati ambapo vikwazo vya nchi za Magharibi vinazidi kuyakandamiza mahusiano yao ya miongo kadhaa.

Moscow imekuwa muuzaji mkuu wa silaha kwa India kwa miongo kadhaa na imesema kuwa inataka kununua bidhaa nyingi zaidi za India ili biashara kati yao ifikie dola bilioni 100 ifikiapo mwaka 2030.

Putin yuko katika ziara yake ya kwanza nchini India kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka minne, wakati ambapo India inafanya mazungumzo na Marekani kwa ajili ya mkataba wa kibiashara, utakaoondoa ushuru mkubwa uliowekwa na Rais Donald Trump katika bidhaa zake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *