Akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz , Netanyahu amesema walijadili jinsi ya kukomesha utawala wa Hamas katika Ukanda wa Gaza na kwamba wamemaliza sehemu ya kwanza.

Pia amesema baada ya muda mfupi wanatarajia kuingia katika awamu ya pili, ambayo ni ngumu zaidi.

Netanyahu amesema atakutana na Rais Donald Trump baadaye mwezi huu, akisema awamu ya pili ya mpango huo wa amani wa Marekani iko karibu.

Waziri huyo Mkuu wa Israel pia amesema kuwa mwishoni mwa mwezi, atakuwa na mazungumzo muhimu sana ya jinsi ya kuhakikisha awamu hiyo ya pili inapata ufanisi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *