Tshisekedi amesema hayo alipowahutubia wabunge hii leo Jumatatu na kuongeza kuwa hatua hiyo inadhoofisha juhudi za kumaliza mapigano mashariki mwa Kongo.

Marais wawili Tshisekedi na Paul Kagame wa Rwanda walisaini makubaliano ya amani mjini Washington wiki iliyopita, mbele ya Rais wa Marekani Donald Trump unaolenga kuumaliza mzozo uliodumu kwa zaidi ya miongo mitatu katika eneo hilo lenye utajiri wa madini.

Hata hivyo kumeripotiwa mapigano makali kwenye eneo hilo licha ya makubaliano hayo, na kulingana na Shirika la Msalaba Mwekundu, karibu raia 20 waliojeruhiwa waliondolewa kati ya Jumamosi na Jumapili kutoka kwenye eneo hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *