Waziri wa Mambo ya Ndani wa Lithuania, Vladislavas Kondratovicius ameliambia Baraza la Mawaziri kwamba hali hiyo ya dharura imetangazwa kutokana na usumbufu wa usafiri wa anga na wasiwasi wa usalama wa taifa.

Mvutano kati ya Lithuania na Belarus umeongezeka baada ya maputo ya hali ya hewa kutoka Belarus kuilazimisha Lithuania kufunga uwanja wake mkuu wa ndege mara kadhaa wiki zilizopita na kukwamisha  maelfu ya watu.

Ingawa maputo hayo hutumiwa kuingiza biashara haramu ya sigara nchini Lithuania, maafisa wa Vilnius wanachukulia kama vitendo vya makusudi vya usumbufu vinavyopangwa na Belarus.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *