Seneti ya Nigeria yaidhinisha wanajeshi wa Tinubu kwenda Benin baada ya jaribio la mapinduzi
Baraza la Seneti la Nigeria siku ya Jumanne lilitoa idhini yake kwa Rais Bola Tinubu kupeleka wanajeshi nchini Benin baada ya serikali ya Rais Patrice Talon kuiomba Nigeria msaada kuzima jaribio la mapinduzi siku ya Jumapili.