
Ofisi ya Rais ya Uturuki imewasilisha rasmi pendekezo bungeni la kutaka kuongezwa kwa muda wa miezi 24 ya kikosi chake cha kijeshi nchini Libya, ikitaja kuendelea kutokuwa na uhakika wa kisiasa, changamoto za kiusalama ambazo hazijatatuliwa na haja ya kuhifadhi utulivu katika nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika.
Hoja hiyo iliyotiwa saini na Rais Recep Tayyip Erdogan, iliwasilishwa kwa Bunge Kuu la Uturuki (TBMM) siku ya Jumapili. Ikiwa itaidhinishwa, mamlaka yataongezwa kutoka Januari 2, 2026, kwa miaka miwili zaidi.
Sababu za kupelekwa kwa jeshi la Uturuki
Hoja hiyo inakujua kufuatia juhudi za awali za kuanzisha taasisi za kidemokrasia nchini Libya kufuatia machafuko yaliyozuka mwaka 2011 zilidhoofishwa na kuongezeka kwa migogoro ya kivita, na kusababisha kugawanyika kwa muundo wa kisiasa na usalama.
Inaashiria Mkataba wa Kisiasa wa Libya, uliotiwa saini huko Skhirat, Morocco, mnamo Desemba 2015, ambao ulisababisha kuundwa kwa serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa inayotambuliwa na jumuiya ya kimataifa chini ya Azimio 2259 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Kulingana na hoja hiyo, mashambulio yaliyoanzishwa mnamo Aprili 2019 yaliyolenga kuangusha serikali inayotambuliwa kimataifa yalisababisha Libya kuomba rasmi msaada kutoka Uturuki mnamo Disemba 2019.
Uturuki inasisitiza umuhimu wa amani na utulivu nchini Libya
Waraka huo unasema huku uwepo wa kijeshi wa Uturuki ulisaidia kusitisha mashambulizi na machafuko ya ndani, Libya bado hakuna usitishaji wa kudumu wa mapigano au kukamilisha mchakato wa mazungumzo ya kisiasa.
Inaonya kwamba kuendelea kutokuwa na uwezo wa kufanya uchaguzi kumeongeza hali ya kutokuwa na uhakika wa kisiasa na changamoto za utawala, na kuweka hatarini utulivu uliopatikana na kuibua wasiwasi wa usalama kwa Libya na eneo zima.
“Kutokuwa na uwezo wa kufanya uchaguzi nchini Libya kumeongeza kutokuwa na uhakika wa kisiasa na matatizo ya utawala, na kuweka hatarini utulivu uliofanikishwa kwa kujitolea sana pamoja na kuweka tishio kubwa kwa utulivu wa kudumu,” hoja hiyo ilisema.
Hoja hiyo inasisitiza kuwa kushindwa kuunganisha taasisi, hasa vyombo vya kijeshi na usalama, bado ni hatari kubwa kwa utulivu wa kudumu.
Jukumu la Uturuki na ushirikiano wa usalama