
Wizara hiyo ilitoa taarifa baada ya Burhan kufanya ziara mjini Riyadh kama mgeni wa Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman, ambaye hivi karibuni aliwasilisha kwa Trump mpango wa amani kwa Sudan wakati wa ziara yake Washington.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Burhan alipongeza “kujitolea kwa Trump kushiriki katika juhudi za kufikia amani na kumaliza vita nchini humo, kwa ushiriki wa Ufalme wa Saudi Arabia.”
Taarifa hiyo pia imesema Burhan alithibitisha ari ya Sudan kufanya kazi na Rais Trump, waziri wake wa mambo ya nje Marco Rubio, na mjumbe wake wa amani nchini Sudan Massad Boulos ili kufikia lengo hilo.