Akieleza tukio hilo kama “baya,” wizara ilitoa wito kwa raia wa Misri “kutohadaiwa na mitandao ya uhamiaji haramu,” ili kulinda maisha yao na kuepuka matukio kama hayo ya uchungu kutokea tena.

Wahamiaji haramu wamekuwa wakitumia Libya na mataifa jirani kufikia kisiwa cha Crete, njia ya kufika nchi za Muungano wa Ulaya.

Mapema mwezi Julai, serikali ya Ugiriki iliamua kufuta maombi ya wanaoomba hifadhi ya kisiasa, hasa wale wanaowasili Crete kutoka Libya.

Misri inasema imezuia kuondoka kwa maboti ya wahamiaji yanayoelekea Ulaya tangu 2016, huku wahamiaji haramu kutoka Misri wakitumia njia ya Libya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *