
Kundi la waasi wa M23 kwa kuutekwa mji wa Uvira hivi kumesababisha watu wengi kuhama makazi yao. Ingawa mapigano bado hayajatokea katika jiji lenyewe, yanaendelea katika sehemu zingine za mkoa wa Kivu Kusini, na kulazimisha raia yahama makazi yao. Kabla ya mpaka wa Burundi kufungwa wiki iliyopita kwa sababu za kiusalama, Wakongo wengi walitafuta hifadhi nchini Burundi, ambapo sasa wanapewa hifadhi katika maeneo yenye msongamano mkubwa. Christina Okello anaripoti.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Walikimbia kwa miguu, wakati mwingine usiku, wakiacha nyumba, mashamba, na mifugo. Mwanzoni mwa mwezi Desemba, familia nzima ziliondoka mashariki mwa DRC ili kutoroka mapigano kati ya AFC/M23 na jeshi la Kongo. Kabla ya kufungwa kwa mpaka wa Burundi, Wakongo elfu kadhaa walivuka kuingia Burundi, haswa kupitia kivuko cha mpaka cha Gatumba. Mamlaka za Burundi zimetenga maeneo kadhaa ili kuwapokea na kuwapa hifadhi.
Lakini, hali ni ngumu sana. Kulingana na ushuhuda, makumi ya maelfu ya familia hukusanyika katika maeneo haya ya muda, mara nyingi bila makazi ya kutosha, maji ya kunywa, au chakula cha kutosha. Kambi kuu ya wakimbizi, iliyoko kwenye kilima kilichozungukwa na mashamba ya chai na inayosaidiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali, ina watu wapatao elfu moja pekee. Tayari imejaa. Kwa hivyo, watu wengi waliokimbia makazi yao wanasubiri kuhamishwa.
Miongoni mwao ni Shukuru Rukara Divin. Asili yake ni kutoka Uwanda wa Ruzizi, alikimbia mapigano na familia yake yote. Anamwambia Christina Okello wa RFI kwa nini ilibidi aondoke, safari ndefu kwa miguu kwenda Burundi, na maisha ya leo katika hali mbaya sana. Anasimulia yaliyomkuta.
RFI: Kwa nini uliamua kuondoka? Nini kilikuwa kikiendelea nyumbani kwako wakati huo?
Shukuru Rukara Divin: “Binafsi, niliondoka na familia yangu yote: mke wangu, watoto wangu, na hata wazazi wangu. Nyumbani, kulikuwa na mabomu, risasi zilikuwa zikitoka kila mahali. Tayari tulikuwa tunaona maiti katika vitongoji tofauti, katika maeneo tofauti. Wakati mwingine, watu walikuwa wakikimbia na kushambuliwa na mabomu na risasi. Kwa kuona haya yote, hatukuwa na chaguo. Tulilazimika kuondoka nyumbani kwetu ili kuepuka kifo.”
RFI: Uliondoka na familia yako yote. Safari ya kwenda Burundi ilikuwaje?
“Safari ilikuwa ngumu sana. Ilikuwa ndefu na ngumu sana. Tuliondoka Luvungi kuelekea Sange kwenda Burundi, kwa miguu. Hebu fikiria kufanya safari hiyo yote kwa miguu. Hakukuwa na njia ya kuchukua pikipiki au gari. Njiani, kulikuwa na majeruhi, hata watoto.” Wakati huo, mpaka ulikuwa bado wazi. Lakini leo, umefungwa kwa sababu za usalama.
RFI: Maisha yako ya kila siku yakoje hapa leo?
“Leo, hali tunazopitia ni ngumu sana. Kwanza kabisa, hakuna makazi. Hatuna nyumba; tunalala nje, katika eneo lisilo na uzio. Kuna ukosefu wa usalama, matatizo ya kiafya. Hakuna vyoo, hakuna maji ya kunywa. Tunakabiliwa na magonjwa. Hata kupata chakula ni tatizo. Hali ya maisha, kijamii na kiuchumi, ni ngumu sana kwetu.”
RFI: Ni wangapi kati yenu mko huko leo, na mnatarajia nini?
“Tuko zaidi ya watu 6,000; idadi hiyo ni kubwa. Tunaishukuru serikali ya Burundi, ambayo ilitupokea bila masharti, bila matatizo yoyote.” Na tunaomba msaada wa kibinadamu utufikie ili tuweze kupata tunachohitaji kuishi, tunachohitaji kula. Tunaomba msaada ili tukidhi mahitaji yetu ya msingi.
Katika upande wa usalama, AFC-M23 imetangaza kujiondoa kutoka Uvira. Mamlaka ya mkoa wa Kivu Kusini inalaani hili kama kujiondoa “kwa uwongo”. Ingawa utulivu umerejea jijini, mapigano yanaendelea kwingineko katika mkoa huo, na kusababisha watu kuenelea kuhama makazi yao.