Mwanza. Tumia pesa Januari isikutishe. Mambo yapo huku yaani ni bata batani. Mwendo wa kufungua vizibo na kula bata hadi kuku waone wivu. Upo Mwanza? Zama maeneo haya ukale bata.

Saanane National Park

Kama wewe ni mdau wa Camping and Bonfire hakikisha mwisho wa mwaka huu, ukiwa Mwanza unatembelea Saanane National Park. Hiki ni kisiwa cha utalii. Utafanya na kuona mengi kama vile wanyama na mengineo.

Satosangara

Bata, ukiwa na familia zama Sato Sangara, huku utapata chakula cha asili ya Kanda ya Ziwa. Chimbo hili ukiwa na familia yako inapendeza zaidi. Hapa ni Restaurant, Bar na VIP Lounge ndani ya Rock City Mall.

The Cask, bar and Grill , Climix ,The kaffeehaous na Grand Prix

Kabla hujaondoka Rock City Mall tembelea The Cask, The Kaffehaus bila kusahau Climix na Grandprix eneo hili utakutana na michezo ya watoto pia.

Kwatunza , Club Elevet Malaika

Ukitaka sehemu ya vibe huku unakula upepo wa Ziwa Victoria pita KwaTunza ipo Ilemela ukiwa unaelekea Airport. Wazee wa kukesha mnaweza kutembelea Club Elevet Malaika hii ni night club ipo Ilemela pia.

Bundesliga Lounge

Watoto wa uswahilini huku ndio kwao sasa na bata la kufa mtu utawakuta Bundesliga Lounge kiwanja hiki kipo Nyasaka. 

BonaSera, Tilapia
Wakishua zama Bona Sera ipo capri point mtaa huu pia kuna chaka jingine liitwalo Tlapia, Bonasera na Rockbeach Garden

Wagi Hill na Elly’s Beach 

Kabla hujaondoka Mwanza pita Wag Hill ipo Nyegezi. Wale wa kupenda maji kama samaki kwenye beach kali zama Elly’s Beach ipo Nyanguge Magu.

Unakosaje kuinjoy na sikukuu hizi za mwisho wa mwaka fuatilia kila nakala zetu kwa mikoa tofauti upate kuzijua sehemu nyeti za kula bata msimu huu, unakaaje kinyonge sasa! Tule bata pamoja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *