Serikali ya Tanzania na India zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) kuhusu ushirikiano kwenye Sekta ya Afya katika kuendeleza tiba asilia (Ayurveda), huku Tanzania ikiwakaribisha wawekezaji kutoka sehemu duniani kuja kuwekeza na kuwahakikishia kuwapatia mazingira mazuri ya uwekezaji.
Utiwaji saini huo kwa upande wa Serikali ya Tanzania umefanywa na Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa na Waziri wa Afya anayeshughulikia Tiba Asili (AYUSH) katika Serikali ya India Mhe. Jagat Prakash Nadda, kwenye Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu Tiba Asilia, uliomalizika hivi kwenye ukumbi wa kimataifa wa Bharat Mandapam jijini New Delhi India.
Aidha, utiwaji saini huo umeshuhudiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus ambapo ameipongeza Serikali ya Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mageuzi makubwa inayofanya kwenye sekta ya afya na kusisitiza kuwa WHO litaendelea kushirikiana kikamilifu.
Mhe. Mchengerwa amesema kusainiwa kwa hati hiyo ya makubaliano ni hatua muhimu kwa Tanzania, kwani kutaimarisha ushirikiano wa kitaasisi na India katika maeneo ya kipaumbele ya sekta ya afya, kuongeza uwezo wa rasilimali watu wa sekta ya afya, kuimarisha udhibiti na matumizi salama ya tiba asilia, pamoja na kuchangia jitihada za Serikali katika kuimarisha mifumo ya huduma za afya na kufikia Bima ya Afya kwa Wote.
“Ushiriki wa Tanzania katika mkutano huu unaakisi dhamira ya Serikali kupitia Wizara ya Afya katika kukuza tiba asilia salama, yenye ushahidi wa kisayansi na inayosimamiwa kwa misingi madhubuti ya udhibiti, sambamba na kuendeleza ushirikiano wa kimataifa kwa maendeleo endelevu ya afya kwa watu wote.” Amesisitiza Waziri Mchengerwa
Tanzania inaendelea kubadilisha tiba asili kutoka katika hekima ya kurithiwa kizazi hadi kizazi, na kuifanya kuwa tiba inayothibitishwa kisayansi, inalindwa kidijitali, na yenye uwezo wa kibiashara kwa manufaa ya afya duniani kote.
“Tunaamini kuwa tiba asi