Lakini pengine swali la Kenya baada ya Odinga ni iwapo kizazi kijacho cha viongozi wa kisiasa, chini ya shinikizo linaloongezeka la wananchi, wanaweza kuona jinsi matamanio yao binafsi yanavyoweza kutimizwa kwa kuitikia matakwa ya wananchi, na si uwezo wao wa kuleta pamoja miungano na mikataba baina yao.

Wataalamu wa masuala ya kisiasa wanasema uchaguzi wa 2027 utakuwa mtihani muhimu.

Huenda Rais Ruto akakabiliwa na changamoto ya kujaribu kuwashawishi Wakenya kwamba anashikilia ahadi alizowaahidi lakini hakuna Rais Kenya aliyewahi kuondoka madarakani kutokana na kushindwa katika uchaguzi. Haijulikani mpinzani wake mkuu atakuwa nani, kwa sababu kwa mara ya kwanza tangu 2002, hatakuwa Raila Odinga.

Wataalamu wengine wanasema kizazi cha vijana maarufu, Gen Z, kimeleta mwelekeo mpya katika siasa.

Bila kutegemea kabila au wanasiasa maarufu, badala yake kudai utoaji wa huduma, wanaweza kusababisha siasa za Kenya kwenye msimamo uliokomaa zaidi.

Swali ni je, vijana hawa wa Kenya wataleta mshikamano na nguvu kwenye sanduku la kura kwa imani kwamba italeta mabadiliko?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *