Makubaliano hayo tete yenye vipengele 20 ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza yalifikiwa Oktoba 10 chini ya uratibu wa Washington yakiwa na lengo la kukomesha mapigano yaliyodumu kwa zaidi ya miaka miwili.

Hata hivyo, utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango huo ambapo Hamas watalazimika kusitisha mapigano na kutumwa kikosi cha kimataifa cha kutuliza hali unatarajiwa kuwa mgumu zaidi na hadi sasa Hamas inaipinga miito yote ya kupokonywa silaha.

Viongozi hao pia watajadiliana kuhusu Iran, ambayo Israel inaituhumu kuwa inaendelea kuongeza akiba yake ya makombora baada ya vita kati ya nchi hizo mbili mapema mwaka huu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *