Mwezi Januari huendelea kutajwa na wengi kama mwezi mgumu, kutokana na shinikizo la maisha linalowakumba wananchi katika kipindi hicho.

Matumizi huongezeka kwa kiasi kikubwa, yakihusisha ada za shule, kodi ya nyumba, pamoja na gharama nyingine za mahitaji ya kila siku.

Mtaalamu wa masuala ya uchumi, Elisante Ephraim, amesema kuwa kukabiliana na changamoto za mwezi Januari kunahitaji nidhamu ya kifedha na uhalisia.

Ameshauri kuwa mtu ambaye hajajiandaa vizuri anapaswa kukubali hali ya kubana matumizi, kuepuka mikopo, na kuacha matumizi yasiyo ya lazima ili kuvuka mwezi huo salama.

✍ Ibrahim Kilumbo
Mhariri | @claud_jm

#AzamTVUpdates

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *