
Akizungumza katika Kaunti ya Uasin Gishu siku ya Jumamosi, Januari 3, Ruto alitetea msimamo wake mkali, akisema yuko tayari kukabiliana na madhara yoyote yatakayojitokeza kutokana na msukumo wa kuanzisha sheria kali zaidi.
Akisema hatua hii inalenga kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya na pombe haramu nchini Kenya.
“Kwa watu wote wanaohusika katika biashara ya pombe haramu, tutabadilisha sheria. Zamani kulikuwa na sheria iliyosema kwamba ukikamatwa ukifanya biashara ya dawa za kulevya, ikiwemo dawa hatari kama heroin, adhabu ilikuwa ni faini ya shilingi milioni moja. Sasa tunabadilisha hilo ili adhabu iwe kunyongwa,” alisema Rais Ruto.
“Mnajua nikisema jambo, nimelisema, na niko tayari kukabiliana na matokeo yake. Tunahitaji kuwa na nidhamu na utaratibu. Familia nyingi sana zinateseka kwa sababu ya kokeini,” aliendelea kusema.