
Na Göktuğ Çalışkan
Huku 2026 ikianza, eneo la Sahel halikabiliani tena na magaidi wanaotoka kwenye jangwa na kushambulia msafara wa magari na kukimbia, mtazamo wa vita umebadilika, kiharakati, na kimkakati.
Katika eneo la Liptako-Gourma, Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES) unakabiliana na tatizo ambalo ni changamoto ambayo siyo tu changamoto kwa taifa, bali lina lengo na kuliondoa taifa.
Mustakbali wa eneo hilo unapatiwa ufumbuzi kwa vita vya nani anatakiwa kuwa uongozini, uwezo, na huduma zinazotolewa.
Kwa upande mwingine, makundi ya kigaidi kama yale yenye uhusiano na Al Qaeda-JNIM na Daesh-GS, yanaendeleza ubabe wake, kwa kuweka hofu, kuweka vizuizi barabarani, na mifumo ya kuamiliana na watu.
Kujidanganya kuhusu mkakati
Tathmini nyingi ya kutoka nje inaonyesha kwa makosa kuwa maeneo ambayo serikali ya Mali au Burkina Faso yanashindwa kufika ni kama “maeneo yasiyoweza kutawaliwa.”
Katika maeneo mengi ya vijijini, kundi la kigaidi la JNIM limetekeleza mfumo mbadala wa uongozi.
Wana mahakama za muda ambazo zinatatua masuala ya ardhi kwa mafanikio na migogoro mingine kati ya wakulima na wafugaji. Ndani ya saa chache, wanatatua, yale ambayo mamlaka za serikali zinaona kama hayawezekani, na yangechukuwa muda wa miezi kadhaa kutatua.
Makundi yenye silaha yanaonekana kama ndiyo yenye “ufumbuzi” wakati taifa linaonekana kama “halipo.”
Ukusanyaji wa kodi pia unamaasha utawala. Kile ambacho kinaonekana kama kurubuniwa kinaleta usalama katika maeneo mengine, na kuwa na mfumo mahsusi, pamoja na ahadi ya kupata ulinzi. Ujumbe uko wazi: serikali inakusanya bila kutoa ahadi zozote za msaada; makundi hayo yanakusanya yakiahidi kuwapa usalama.