
Bei ya mafuta yashuka kidogo leo Jumatano baada ya Donald Trump kutangaza siku ya Jumanne kwamba Venezuela “itakabidhi” hadi mapipa milioni 50 ya mafuta kwa Marekani. Hii inakuja huku mvutano ukiongezeka nchini Venezuela kufuatia mashambulizi ya Marekani usiku wa Ijumaa, Januari 2, na kutekwa nyara kwa Nicolas Maduro. Kwa kuwa hali ya hatari sasa inaanza, makundi ya wanamgambo yanayounga mkono utawala vimepelekwa katika mitaa ya Caracas.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Caracas na Washington wamefikia makubaliano ya usafirishaji wa mamilioni ya mapipa ya mafuta ya Venezuela kwenda Marekani, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza siku ya Jumanne, Desemba 6.
Bei ya mafuta yashuka kidogo Jumatano kufuatia kauli ya Donald Trump siku ya Jumanne kwamba Venezuela “itakabidhi” hadi mapipa milioni 50 ya mafuta kwa Marekani. Karibu saa 11:40 mchana saa za Ufaransa, bei ya mafuta ghafi ya Brent kutoka Bahari ya Kaskazini, kwa ajili ya usafirishaji wa Machi, ilishuka kwa 0.44% kwa dola 60.43 kwa pipa. Sawa na Marekani, West Texas Intermediate, kwa usafirishaji mwezi Februari, imeshuka kwa 0.75% kwa dola 56.70 kwa pipa.
Jambo jingine lililochangia kupungua ni mazungumzo ya yanayoendelea kati ya Kyiv na wajumbe wa Marekani huko Paris kuhusu usitishaji mapigano nchini Ukraine, ambao bado ni matarajio makubwa kwa pande wa Urusi, baada ya kukubaliana siku iliyopita, pamoja na viongozi wa Ulaya, kuhusu seti ya dhamana za usalama kwa Ukraine.
Rais Donald Trump anadai kwamba Caracas itasafirisha “kati ya mapipa milioni 30 na 50 ya mafuta” kwenda Marekani, alisema siku ya Jumanne, Desemba 6, katika chapisho kwenye mtandao wake wa Truth Social. Usafirishaji huu wa mafuta unawakilisha karibu miezi miwili ya uzalishaji wa Venezuela na unakadiriwa kuwa na thamani kati ya dola milioni 1.8 na dola bilioni 3. Anadai kwamba kiasi hiki kitadhibitiwa kibinafsi na Trump ili kuhakikisha “kwamba kinatumika kwa manufaa ya raia wa Marekani na Venezuela.”
Hadi sasa hakuna maoni yoyote kutoka Caracas, wala kutoka kwa mamlaka wala kutoka kwa kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali, Petroleo de Venezuela SA. Bado ni vigumu kuona kile ambacho Venezuela inapata kutokana na makubaliano haya zaidi ya nia ya serikali ya Delcy Rodriguez ya kuonyesha kwamba inakubali vitisho vya mara kwa mara kutoka Washington.
Uzalishaji wa mafuta wa Venezuela ni mdogo: chini ya mapipa milioni moja kwa siku. Kwa hivyo, mapipa haya milioni 30 hadi 50 yatatoka wapi? Tangazo la Donald Trump halitoi maelezo yoyote. Lakini tangu katikati ya mwezi Desemba na kizuizi kilichowekwa na Washington, kiasi kikubwa kimehifadhiwa katika meli za mafuta na bandari nchini Venezuela.