Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatano, Marekani imesema imepokea ripoti kuwa maafisa wa Somalia waliharibu ghala la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, lililofadhiliwa na Marekani na kuchukua kinyume cha sheria tani 76 za chakula kilichokusudiwa kwa wananchi walio hatarini.

Marekani imesisitiza kuwa ina sera ya kutovumilia kabisa wizi au upotevu wa misaada na kwamba msaada wowote wa baadaye utategemea uwajibikaji wa serikali ya Somalia. Hata hivyo maafisa wa Somalia hawajatoa jibu rasmi kuhusu hatua ya Marekani.

Somalia, iliyopo katika Pembe ya Afrika, inaendelea kukabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama na kiuchumi, huku Umoja wa Mataifa ikiiorodhesha miongoni mwa nchi masikini zaidi duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *