
Takribani kaya 45,000 na biashara 2,200 zilijikuta gizani mapema Jumamosi baada ya nyaya za umeme zenye voltage kubwa kuchomwa moto, jambo lililoibua maswali kuhusu uimara wa Ujerumani dhidi ya hujuma kwenye miundombinu yake muhimu. Shambulio hilo lilisababisha pia kufungwa kwa shule na hospitali, lilidaiwa kufanywa na kundi la wanaharakati linalojiita Vulkangruppe (Kundi la Volcano).Tukio hili linakuja wakati ambapo Ujerumani, mdhamini mkubwa wa Ukraine, imeshutumu Urusi kwa mashambulizi ya tofauti, kuanzia ya droni na ujasusi hadi upotoshaji mtandaoni. Hata hivyo jana Jumatano, msemaji wa wizara ya mambo ya ndani alisema hakuna dalili kwamba Urusi ilihusika.