Maandamano hayo yaliyoandaliwa na vyama vya wafanyakazi vya Afrika Kusini, vyama vya kisiasa, vyama vya wanafunzi na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yaliungwa mkono na watu wengi waliokusanyika nje ya ubalozi wa Marekani.

Solly Mapaila, katibu mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Afrika Kusini (SACP),alishtumu kile alichokisema uingiliaji wa masuala ya ndani ya nchi ya Venezuela kwa Marekani na kutaka Maduro na mkewe waachiliwe bila masharti yoyote.

“Muachilie huru Rais Nicholas Maduro, Muachilie huru Cilia Flores, hatutaki ukoloni, maisha marefu kwa Venezuela,” alisikika akiwa pamoja na waandamanaji waliokuwa wamevaa fulana nyekundu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *