Maafisa wa ngazi ya juu katika wizara hiyo wameliambia shirika la habari la Reuters kwamba sababu ya kuahirishwa kwa ziara ya Wang Yi nchini Somalia na tarehe nyingine itakapofanyika, itatolewa baadaye.

Wang Yi alikutana na waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed Alhamisi na kutoa wito pawepo ushirikiano mkubwa zaidi na nchi hiyo ya Afrika ambayo uchumi wake unakua kwa kasi kabisa, ikiwemo miundombinu, nishati safi isiyochafua mazingira na uchumi wa kidijitali.

Wang Yi alikutana na Abiy mjini Addis Ababa katika kituo chake cha kwanza cha ziara yake ya kila mwaka ya mwaka mpya ya siku sita hadi Januari 12 barani Afrika, itakayompeleka pia Tanzania na Lesotho.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *